Housigeli asimulia jinsi alivyoutoa uhai wa mtoto wa jirani!!!!

0 comments


MSICHANA wa kazi ‘hausigeli’ aitwaye Enjoy Cleofasi (19), hivi karibuni alipandisha mapepo na kumtwanga mwandishi wa habari aliyekuwa akimhoji kuhusiana na tukio la mauaji lililotokea mjini Dodoma
Tukio hilo la kukunjwa kwa mwandishi, lilitokea juzikati Kipunguni jijini Dar wakati Enjoy alipokuwa akisimulia jinsi alivyoutoa uhai wa mtoto wa jirani wakati alipokuwa akifanya kazi za ndani mkoani Dodoma.
Wakati Enjoy akisimulia mkasa huo, ghafla  alibadilika na kuanza kuweweseka huku akionekana kama mgonjwa kisha kumkwida shati mwandishi (jina tunalo) ambaye naye alilazimika kukabana naye na kujitoa mikononi mwake.
Timbwili zito likazuka kiasi cha kuwafanya baadhi ya watu waliokuwa eneo la tukio kukimbia kwa kuhofia mapepo ya msichana huyo.
Msichana huyo akisimulia alivyoutoa uhai wa mtoto wa jirani mjini Dodoma, alisema matatizo yalianza baada ya kumuona mwanamke aliyemtokea katika mazingira ya kutatanisha akiwa shuleni mjini humo.
“Mwanamke huyo alitokea kwenye maua na  kuniita huku akiniambia ametokea kunipenda na kunitaka nimfuate, nilikataa ghafla nikawa sijielewi kisha nikapoteza fahamu,” alisema msichana huyo na kudai kwamba alikuja kuzinduka akiwa ofisini kwa walimu wake akiwa hakumbuki chochote.

Baada ya tukio hilo, Enjoy alisema mwanamke huyo alimfuata tena usiku huku akiwa ananukia marashi, akiwa amevaa nguo nyeupe ilhali akiwa haonekani chini ya miguu yake na kujitambulisha kwa jina la Shakira.
 “Mwanamke huyo aliniambia kwamba yuko na wenzake, wametumwa kunichukua kwa sababu nina akili sana nikafanye kazi zao lakini nilikataa,” alisema Enjoy.
Kutokana na mfululizo wa matukio hayo, Enjoy alisema alilazimika kubadili dini na kuwa Muislamu na kupewa jina la Jamila na Shehe aliyefika nyumbani kwako kumsomea dua.
Jamila alisema baada ya kutibiwa na shehe huyo alipona na kuanza kwenda shule, safari hii akajiunga na shule ya bweni.
Aliongeza kuwa, siku moja akiwa amelala usiku alishtuka na kukiona kitanda chote kikiwa kimelowa damu kiasi cha kutisha.
Alisema alipiga kelele lakini haikusaidia kitu, walimu walipoiona hali hiyo walimrudisha nyumbani kwa ajili ya kupata matibabu.
 “Nilitibiwa na kurudi shule lakini nikiwa darasani nikawa naona giza, hivyo nikashindwa kuendelea na masomo. Nilirudi  nyumbani kisha nikapata kazi ya ndani hapohapo Dodoma huku mauzauza yakiendelea,” alisema.
Akiendelea kufanya kazi siku moja usiku alimuota tena yule mwanamke akiwa amemtokea na kumkabidhi kisu akimtaka akamuue mtoto mdogo wa jirani.
“Nikiwa ndotoni niliota ninachukua kile kisu na kwenda kumchoma mtoto yule shingoni, cha ajabu wakati nikimchoma damu haikutoka baada ya hapo nikapewa kiapo nikitakiwa kuitunza siri hiyo la sivyo nitakiona cha moto,” alisema Enjoy.
Akiendelea kusimulia msichana huyo alisema kuwa, asubuhi alipata taarifa kwamba yule mtoto wa jirani aliyemuota usiku amefariki dunia kwa kuchomwa na kisu.
“Kilichonishtua zaidi ni pale majirani waliposema kwamba pamoja na mtoto huyo kuchomwa kisu, damu haikuonekana hata chembe ingawa jeraha lilionekana shingoni,” alisema Enjoy kwa majonzi.
Enjoy alisema kuwa aliendelea kuitunza siri hiyo huku mauzauza yakiendelea na baada ya muda aliamua kuacha kazi na kuhamia Kipunguni Dar kwa dada aitwaye Regina Msafiri aliyeamua kumsaidia.
chanzo:globalpublishers

Read More »

MTOTO AFICHUA SIRI NZITO YA ASKARI ALIEMUUA BABA YAKE MZAZI

0 comments
Kamanda wa Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova





*Familia yachachamaa yataka uchunguzi huru
KUNDI la polisi wasiojulikana kwa mara nyingine wameendelea kulipaka matope jeshi hilo baada ya kutajwa kuhusika katika mauaji mengine ya raia wakati akiwa katika mikono yao. Tukio hilo jipya na la aina yake limefichuliwa na mtoto wa marehemu ambaye alisema, kabla ya kufikwa na mauti baba yake, alikamatwa na kupigwa na polisi katika maeneo ya Kurasini jijini Dar es Salaam.
Taarifa za polisi kuhusika na mauaji ya mwananchi huyo aliyetajwa kwa jina la Selemani Mwinyimsanga mwenye umri wa kati ya miaka 35 na 40 zilitolewa kwa mara ya kwanza na mtoto wa marehemu ambaye alishuhudia askari hao wakimpa kipigo baba yake. Kuvuja kwa taarifa hizo za polisi kuhusishwa na tukio hilo, kulielezwa jana na binamu wa marehemu, Joachim Mgembe wakati alipozungumza na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam.
Akisimulia mkasa huo uliotokea Jumanne ya wiki iliyopita, Mgembe alimkariri mtoto huyo wa marehemu ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha tatu aliyemtaja kwa jina moja la Geoffrey akisema aliona namna baba yake alivyokuwa amedhoofika baada ya kipigo hicho.
“Nilipata taarifa juzi kutoka kwa mtoto wa kaka wa marehemu anayeitwa,Nasoro Hamadi, kuwa baba yake mdogo ambaye ni marehemu, amefariki dunia.
“Alinieleza kuwa, Selemani alikamatwa na polisi katika eneo ambalo halikufahamika na kisha askari hao wakamchukua na kumpeleka nyumbani kwake Kurasini.
“Walipomfikisha nyumbani kwake, walianza kupekua ndani na inaonekana hawakukuta kitu.
“Baada ya upekuzi huo, wakaanza kumpiga, inasemekana walimpiga sana hadi akadhoofika na kwa bahati nzuri wakati wanampiga marehemu, alikuwapo mtoto wa mke wake anayeitwa,.
Mgembe alimkariri mtoto huyo akisema mara baada ya kipigo hicho polisi hao waliondoka na baba yake na wakaenda naye eneo lisilojulikana.
Alisema mara tu baada ya tukio hilo, kijana huyo alimpigia simu mama yake akimueleza kuhusu kile kilichotokea. Mawasiliano hayo yalisababisha mke huyo wa marehemu kurejea nyumbani kwa dharura na kutoa taarifa kwa ndugu na jamaa zake kabla ya kuanza kumtafuta mumewe katika vituo mbalimbali ya polisi.
Kwa mujibu wa Mgembe, polisi hao walimchukua marehemu hadi kituo cha polisi cha Oysterbay ambako inadaiwa marehemu akiwa hapo kabla mauti kumfika aliwasiliana kwa simu na dada yake kwa njia ya simu akimueleza namna alivyopigwa na polisi kwa kiwango cha kuhitaji msaada wa matibabu.
“Ndugu walikwenda pale Polisi Oysterbay ili kumdhamini lakini walipofika kituoni hapo, waliambiwa hakukuwa na taarifa za ndugu yetu na wakawashauri waende Kituo cha Polisi, Stakishari Ukonga ambako ndiko walikohisi marehemu angeweza kukutwa.
“Ndugu zangu hawakukata tamaa, walikwenda Stakishari, ambako nako hawakuambulia kitu zaidi ya kupewa majibu kuwa hawajamkamata mtu wa namna hiyo.
Baada ya majibu hayo, Mgembe alisema majibu hayo yalisababisha ndugu hao kurejea tena Polisi Oysterbay ambako ndugu yao aliwaeleza awali kwamba ndiko alikokuwa akishikiliwa. Wakiwa kituoni hapo, Mgembe anasema ndipo baadhi ya askari polisi wawili ambao hawakuweza kuwataja walipowaeleza kwamba ndugu yao waliyekuwa wakimtafuta alipoteza maisha kutokana na kipigo.
“Walipokuwa kituoni hapo, waliibiwa siri na askari wawili waliokutana nao kwenye ngazi na kuambiwa kuwa, ndugu yetu alifikishwa kituoni hapo, lakini kutokana na kipigo alichokuwa amepata, alikuwa amefariki dunia.
Mgembe alisema taarifa hizo zilisababisha dada wa marehemu kuangua kilio hapo hapo, tukio lililosababisha polisi waliofichua siri hiyo kutoweka, pengine kwa kuhofia usalama wao wa kikazi baada ya kufichua siri hiyo.
Baada ya taarifa hizo, ndugu wa marehemu walianza kuzunguka katika hospitali mbalimbali kumtafuta ndugu yao, wakianzia na Hospitali ya Taifa Muhimbili ambako hawakufanikiwa. Baada ya kutoka hapo, walikwenda katika hospitali ya Mwananyamala, ambako walikuta mwili wa marehemu ndugu yao.
Akizungumzia tukio hilo, kaka mwingine wa marehemu, Hassan Mwinyimsanga alitaka uchunguzi ufanywe kuhusu mazingira tatanishi ya kifo cha ndugu yake. Gazeti hili lilipowasiliana na Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Kinondoni, Camilius Wambura, alisema hakuwa na taarifa zozote za kuwapo kwa tukio la namna hiyo na akaahidi kulifuatilia.
Majibu hayo ya RPC Wambura yalisababisha gazeti hili kuwasiliana na Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova ambaye naye alishindwa kueleza lolote kutokana na kuwa likizo. Badala yake, Kamanda Kova alilitaka gazeti hili kuwasiliana na viongozi wengine wa jeshi hilo.

Read More »

RAY C NA KAULI YAKE KUHUSU RECHO KUCOPY STYLE YAKE YA UIMBAJI....!!!

0 comments
Mwanamuziki wa kitambo Rehema Chalamila maarufu kama Ray C ana matarajio ya kurudi katika game baada ya kuwa fiti sasa kiafya. Kupitia mtandao wa instragram Ray C amekuwa akitupia picha zinazomuonyesha akiwa na afya nzuri tena kanona si haba!


Watu wengi wamekuwa wakimuhoji kupitia mtandao huo kuhusiana na mwanamuziki Recho kutumia style inayofanana na Ray C kama anafurahia au lah huku kukiwa na nmafikirio huenda hapendezwi na kitu hicho lakini ukweli ni kuwa Ray C anamfurahia na hivi karibuni wanarajia kudondosha kolabo kwa mujibu wa alichokiandika Instagram.
Alianza kwa kupost picha ya Recho..


Kisha akaandika maelezo..



Katika interview kadhaa Recho ameshawahi kukiri kuwa alivutiwa na Ray C kuingia katika muziki na ni mmoja katika ya wanamuziki anaowazimia mpaka leo na ndio maana style zao za  uimbaji na uchezaji zinafanana.Ray C pia aliwahi kuandika ujumbe wa kuwashukuru mashabiki wake kwa kumsapoti alipopata matatizo ya kiafya mpaka leo.

Najaribu kuvuta picha ya kolabo ya wawili hawa halafu siipati hiyo picha yenyewe

Read More »

Unyama: Binti aoza sehemu za siri amiminika usaha, baada ya kubakwa na kulatiwa

0 comments
Mabinti wa kazi ni sehemu ya familia zetu kutokana na majukumu ya nyumbani tunayoawaachia ikiwemo mapishi,malezi ya watoto,uangalizi wa nyumba n.k. Tunaaswa kila mara kuishi nao vizuri maana nao ni binadamu na wanahitaji upendo. Si kila mtu analitambua hili,ukatili na unyama kwa mabinti hao umeendelea kushika kasi kila kukicha!
Binti mmoja (jina tunalo) kutoka Mtwara aliyeletwa Dar es salaam kuja kufanya kazi amejikuta kwenye mateso makali baada ya kutelekezwa bila nauli na kukutana na fataki aliomshawishi na kumuweka kinyumba na kusababisha majanga hayo yaliyofanya nimweke kwenye blog hii.




Akizungumza na Hatua Tatu ya Times fm Binti huyo amesema,Akiwa na umri wa miaka kumi na tano (15) tu, alitolewa kwao Mtwara na kuletwa hapa Dar na dada mmoja aliyemtaja kwa jina moja la Sophia kwa ajili ya usaidizi wa kazi za ndani.Kwa maelezo yake ilitokea siku alimchapa mtoto wa bosi wake ndipo bosi alipokasirika na kufikia hatua ya kumtimua bila ya kumpa nauli ya kurudia kwao.

Alikutana na baba mwenye mke na watoto wa nne akamshawishi atampa maisha mazuri, akamweka kinyumba na kuanza kumtumia kimapenzi kinyume na maumbile. Kutokana na umri mdogo alionao,ilimsababishia kuharibika sehemu zake za siri na baba huyo na kumtelekeza baada ya kumtomlipia kodi sehemu aliyompangia chumba na majirani wa hapo ndio waliomsaidia.


Hivi sasa binti huyo ameoza sehemu zake za siri anamiminika usaha tu na amehifadhiwa hospitali ya Amana anakopatiwa matibabu na misaada midogo kama chakula.Cha kusikitisha zaidi baada ya kupimwa kakutwa na Ujauzito wa miezi mitatu na kapimwa virusi vya UKIMWI ambapo Vipimo vinatoka leo alhamisi kujua kama kaathirika au la.

Baada ya leo nitakupa jibu nini kimeendelea kuhusu vipimo na jinsi ya kumpa  msaada binti huyu. Pia unaweza kumsikiliza leo Alhamisi na kesho kupitia Radio Times ndani ya kipindi cha  Hatua Tatu.


Source: mamuafrica

Read More »

HUYU NDIYE MWANAUME PEKEE AMBAYE HAJAWAHI KUOGA WALA KUKATA NDEVU

0 comments
Mr Singh na Mkewe
Hakika haya tunaweza kuyaita mafanikio ya ajabu kwa mzee huyu kutokana maamuzi yake.Labda tumite Mr Adui wa Maji ila jina lake kamili ni Mr Kailash Singh akiwa na ndiye anayeshikilia rekodi ya mtu anayenuka zaidi kutokana na kutokuoga kwa zaidi ya miaka 37 sasa.

Mr Singh, 65, hajaoga na hata kukata nywele zake zenye urefu wa futi 6 toka mwaka 1974, mda mfupi mara baada ya kutoka kuoa.

Akielezea juu ya uamuzi wake wakushangaza, Mr Singh anasema mchungaji alimuahidi zawadi ya mtoto wa kiume kama atafata ushauri.

Licha ya majirani kuwa wanamtania na kumdhihaki jamaa huyo walishindwa kubadili maamuzi yake na namna ya kipekee alifanikiwa kumshawishi mke wake, ila cha ajabu zaidi ni pale ambapo imani yake imeonekana kumdanganya kwani ameishia kupata watoto saba ambao wote ni wa kike.

Source:Dan Chibo

Read More »

JOKATE, MUSSA KIPANYA WAZUA JAMBO

0 comments
MWANAMITINDO na mtangazaji maarufu Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ na Mtangazaji Mussa wa runinga wamezua jambo kufuatia picha zinazodhihirisha urafiki wao uliodumu kwa zaidi ya miaka kumi kunaswa.
Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ katika pozi na Mtangazaji Mussa.
Awali paparazi wetu aliinasa picha ya wawili hao ambayo kwa mujibu wao, walipiga miaka kumi iliyopita na walipokutana tena mwaka huu wakapiga mpya.
Baadhi ya wadau walioziona kwa mara ya kwanza, waliibua minong’ono kuwa urafiki wao ni wa siku nyingi hivyo kuna uwezekano wakafikia hatua ya ndoa.
 
Musa na Jokate katika picha ambayo inadaiwa kupigwa miaka kumi iliyopita.
“Urafiki wao ni wa kitambo, wanaweza kuja kuoana kabisa sababu aina ya maisha yao ni ya usiri sana,” alisema mdau mmoja ingawa wenyewe wamesema hawana cha kuzungumza juu ya hilo.

Read More »