"SINA MPANGO WA KUZAA"... JACK PATRICK

Akichonga na paparazi wetu juzikati jijini Dar, Jack alisema kwa sasa yeye na kuzaa mbalimbali kwa vile ana mipango mingi ya maisha ingawaje anapenda sana watoto.
“Napenda sana watoto lakini sitarajii kabisa kuzaa kesho wala keshokutwa, kwasababu ni lazima ujipange sawasawa ili uweze kumtunza vyema mtoto pindi utakapojifungua,” alisema na kuongea:

 
“Wanawake wengi wanaharakisha kuzaa matokeo yake ni kuwaacha watoto nyumbani na mahausigeli wakiwa wadogo ili wao wakatafute chochote,  lazima ukae na mwanao hata mwaka mmoja aweze kupata malezi bora ndiyo maana nasema lazima ujipange sana.”

0 comments: