Showing posts with label matukio. Show all posts

Housigeli asimulia jinsi alivyoutoa uhai wa mtoto wa jirani!!!!

0 comments


MSICHANA wa kazi ‘hausigeli’ aitwaye Enjoy Cleofasi (19), hivi karibuni alipandisha mapepo na kumtwanga mwandishi wa habari aliyekuwa akimhoji kuhusiana na tukio la mauaji lililotokea mjini Dodoma
Tukio hilo la kukunjwa kwa mwandishi, lilitokea juzikati Kipunguni jijini Dar wakati Enjoy alipokuwa akisimulia jinsi alivyoutoa uhai wa mtoto wa jirani wakati alipokuwa akifanya kazi za ndani mkoani Dodoma.
Wakati Enjoy akisimulia mkasa huo, ghafla  alibadilika na kuanza kuweweseka huku akionekana kama mgonjwa kisha kumkwida shati mwandishi (jina tunalo) ambaye naye alilazimika kukabana naye na kujitoa mikononi mwake.
Timbwili zito likazuka kiasi cha kuwafanya baadhi ya watu waliokuwa eneo la tukio kukimbia kwa kuhofia mapepo ya msichana huyo.
Msichana huyo akisimulia alivyoutoa uhai wa mtoto wa jirani mjini Dodoma, alisema matatizo yalianza baada ya kumuona mwanamke aliyemtokea katika mazingira ya kutatanisha akiwa shuleni mjini humo.
“Mwanamke huyo alitokea kwenye maua na  kuniita huku akiniambia ametokea kunipenda na kunitaka nimfuate, nilikataa ghafla nikawa sijielewi kisha nikapoteza fahamu,” alisema msichana huyo na kudai kwamba alikuja kuzinduka akiwa ofisini kwa walimu wake akiwa hakumbuki chochote.

Baada ya tukio hilo, Enjoy alisema mwanamke huyo alimfuata tena usiku huku akiwa ananukia marashi, akiwa amevaa nguo nyeupe ilhali akiwa haonekani chini ya miguu yake na kujitambulisha kwa jina la Shakira.
 “Mwanamke huyo aliniambia kwamba yuko na wenzake, wametumwa kunichukua kwa sababu nina akili sana nikafanye kazi zao lakini nilikataa,” alisema Enjoy.
Kutokana na mfululizo wa matukio hayo, Enjoy alisema alilazimika kubadili dini na kuwa Muislamu na kupewa jina la Jamila na Shehe aliyefika nyumbani kwako kumsomea dua.
Jamila alisema baada ya kutibiwa na shehe huyo alipona na kuanza kwenda shule, safari hii akajiunga na shule ya bweni.
Aliongeza kuwa, siku moja akiwa amelala usiku alishtuka na kukiona kitanda chote kikiwa kimelowa damu kiasi cha kutisha.
Alisema alipiga kelele lakini haikusaidia kitu, walimu walipoiona hali hiyo walimrudisha nyumbani kwa ajili ya kupata matibabu.
 “Nilitibiwa na kurudi shule lakini nikiwa darasani nikawa naona giza, hivyo nikashindwa kuendelea na masomo. Nilirudi  nyumbani kisha nikapata kazi ya ndani hapohapo Dodoma huku mauzauza yakiendelea,” alisema.
Akiendelea kufanya kazi siku moja usiku alimuota tena yule mwanamke akiwa amemtokea na kumkabidhi kisu akimtaka akamuue mtoto mdogo wa jirani.
“Nikiwa ndotoni niliota ninachukua kile kisu na kwenda kumchoma mtoto yule shingoni, cha ajabu wakati nikimchoma damu haikutoka baada ya hapo nikapewa kiapo nikitakiwa kuitunza siri hiyo la sivyo nitakiona cha moto,” alisema Enjoy.
Akiendelea kusimulia msichana huyo alisema kuwa, asubuhi alipata taarifa kwamba yule mtoto wa jirani aliyemuota usiku amefariki dunia kwa kuchomwa na kisu.
“Kilichonishtua zaidi ni pale majirani waliposema kwamba pamoja na mtoto huyo kuchomwa kisu, damu haikuonekana hata chembe ingawa jeraha lilionekana shingoni,” alisema Enjoy kwa majonzi.
Enjoy alisema kuwa aliendelea kuitunza siri hiyo huku mauzauza yakiendelea na baada ya muda aliamua kuacha kazi na kuhamia Kipunguni Dar kwa dada aitwaye Regina Msafiri aliyeamua kumsaidia.
chanzo:globalpublishers

Read More »

MTOTO AFICHUA SIRI NZITO YA ASKARI ALIEMUUA BABA YAKE MZAZI

0 comments
Kamanda wa Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova





*Familia yachachamaa yataka uchunguzi huru
KUNDI la polisi wasiojulikana kwa mara nyingine wameendelea kulipaka matope jeshi hilo baada ya kutajwa kuhusika katika mauaji mengine ya raia wakati akiwa katika mikono yao. Tukio hilo jipya na la aina yake limefichuliwa na mtoto wa marehemu ambaye alisema, kabla ya kufikwa na mauti baba yake, alikamatwa na kupigwa na polisi katika maeneo ya Kurasini jijini Dar es Salaam.
Taarifa za polisi kuhusika na mauaji ya mwananchi huyo aliyetajwa kwa jina la Selemani Mwinyimsanga mwenye umri wa kati ya miaka 35 na 40 zilitolewa kwa mara ya kwanza na mtoto wa marehemu ambaye alishuhudia askari hao wakimpa kipigo baba yake. Kuvuja kwa taarifa hizo za polisi kuhusishwa na tukio hilo, kulielezwa jana na binamu wa marehemu, Joachim Mgembe wakati alipozungumza na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam.
Akisimulia mkasa huo uliotokea Jumanne ya wiki iliyopita, Mgembe alimkariri mtoto huyo wa marehemu ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha tatu aliyemtaja kwa jina moja la Geoffrey akisema aliona namna baba yake alivyokuwa amedhoofika baada ya kipigo hicho.
“Nilipata taarifa juzi kutoka kwa mtoto wa kaka wa marehemu anayeitwa,Nasoro Hamadi, kuwa baba yake mdogo ambaye ni marehemu, amefariki dunia.
“Alinieleza kuwa, Selemani alikamatwa na polisi katika eneo ambalo halikufahamika na kisha askari hao wakamchukua na kumpeleka nyumbani kwake Kurasini.
“Walipomfikisha nyumbani kwake, walianza kupekua ndani na inaonekana hawakukuta kitu.
“Baada ya upekuzi huo, wakaanza kumpiga, inasemekana walimpiga sana hadi akadhoofika na kwa bahati nzuri wakati wanampiga marehemu, alikuwapo mtoto wa mke wake anayeitwa,.
Mgembe alimkariri mtoto huyo akisema mara baada ya kipigo hicho polisi hao waliondoka na baba yake na wakaenda naye eneo lisilojulikana.
Alisema mara tu baada ya tukio hilo, kijana huyo alimpigia simu mama yake akimueleza kuhusu kile kilichotokea. Mawasiliano hayo yalisababisha mke huyo wa marehemu kurejea nyumbani kwa dharura na kutoa taarifa kwa ndugu na jamaa zake kabla ya kuanza kumtafuta mumewe katika vituo mbalimbali ya polisi.
Kwa mujibu wa Mgembe, polisi hao walimchukua marehemu hadi kituo cha polisi cha Oysterbay ambako inadaiwa marehemu akiwa hapo kabla mauti kumfika aliwasiliana kwa simu na dada yake kwa njia ya simu akimueleza namna alivyopigwa na polisi kwa kiwango cha kuhitaji msaada wa matibabu.
“Ndugu walikwenda pale Polisi Oysterbay ili kumdhamini lakini walipofika kituoni hapo, waliambiwa hakukuwa na taarifa za ndugu yetu na wakawashauri waende Kituo cha Polisi, Stakishari Ukonga ambako ndiko walikohisi marehemu angeweza kukutwa.
“Ndugu zangu hawakukata tamaa, walikwenda Stakishari, ambako nako hawakuambulia kitu zaidi ya kupewa majibu kuwa hawajamkamata mtu wa namna hiyo.
Baada ya majibu hayo, Mgembe alisema majibu hayo yalisababisha ndugu hao kurejea tena Polisi Oysterbay ambako ndugu yao aliwaeleza awali kwamba ndiko alikokuwa akishikiliwa. Wakiwa kituoni hapo, Mgembe anasema ndipo baadhi ya askari polisi wawili ambao hawakuweza kuwataja walipowaeleza kwamba ndugu yao waliyekuwa wakimtafuta alipoteza maisha kutokana na kipigo.
“Walipokuwa kituoni hapo, waliibiwa siri na askari wawili waliokutana nao kwenye ngazi na kuambiwa kuwa, ndugu yetu alifikishwa kituoni hapo, lakini kutokana na kipigo alichokuwa amepata, alikuwa amefariki dunia.
Mgembe alisema taarifa hizo zilisababisha dada wa marehemu kuangua kilio hapo hapo, tukio lililosababisha polisi waliofichua siri hiyo kutoweka, pengine kwa kuhofia usalama wao wa kikazi baada ya kufichua siri hiyo.
Baada ya taarifa hizo, ndugu wa marehemu walianza kuzunguka katika hospitali mbalimbali kumtafuta ndugu yao, wakianzia na Hospitali ya Taifa Muhimbili ambako hawakufanikiwa. Baada ya kutoka hapo, walikwenda katika hospitali ya Mwananyamala, ambako walikuta mwili wa marehemu ndugu yao.
Akizungumzia tukio hilo, kaka mwingine wa marehemu, Hassan Mwinyimsanga alitaka uchunguzi ufanywe kuhusu mazingira tatanishi ya kifo cha ndugu yake. Gazeti hili lilipowasiliana na Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Kinondoni, Camilius Wambura, alisema hakuwa na taarifa zozote za kuwapo kwa tukio la namna hiyo na akaahidi kulifuatilia.
Majibu hayo ya RPC Wambura yalisababisha gazeti hili kuwasiliana na Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova ambaye naye alishindwa kueleza lolote kutokana na kuwa likizo. Badala yake, Kamanda Kova alilitaka gazeti hili kuwasiliana na viongozi wengine wa jeshi hilo.

Read More »

Unyama: Binti aoza sehemu za siri amiminika usaha, baada ya kubakwa na kulatiwa

0 comments
Mabinti wa kazi ni sehemu ya familia zetu kutokana na majukumu ya nyumbani tunayoawaachia ikiwemo mapishi,malezi ya watoto,uangalizi wa nyumba n.k. Tunaaswa kila mara kuishi nao vizuri maana nao ni binadamu na wanahitaji upendo. Si kila mtu analitambua hili,ukatili na unyama kwa mabinti hao umeendelea kushika kasi kila kukicha!
Binti mmoja (jina tunalo) kutoka Mtwara aliyeletwa Dar es salaam kuja kufanya kazi amejikuta kwenye mateso makali baada ya kutelekezwa bila nauli na kukutana na fataki aliomshawishi na kumuweka kinyumba na kusababisha majanga hayo yaliyofanya nimweke kwenye blog hii.




Akizungumza na Hatua Tatu ya Times fm Binti huyo amesema,Akiwa na umri wa miaka kumi na tano (15) tu, alitolewa kwao Mtwara na kuletwa hapa Dar na dada mmoja aliyemtaja kwa jina moja la Sophia kwa ajili ya usaidizi wa kazi za ndani.Kwa maelezo yake ilitokea siku alimchapa mtoto wa bosi wake ndipo bosi alipokasirika na kufikia hatua ya kumtimua bila ya kumpa nauli ya kurudia kwao.

Alikutana na baba mwenye mke na watoto wa nne akamshawishi atampa maisha mazuri, akamweka kinyumba na kuanza kumtumia kimapenzi kinyume na maumbile. Kutokana na umri mdogo alionao,ilimsababishia kuharibika sehemu zake za siri na baba huyo na kumtelekeza baada ya kumtomlipia kodi sehemu aliyompangia chumba na majirani wa hapo ndio waliomsaidia.


Hivi sasa binti huyo ameoza sehemu zake za siri anamiminika usaha tu na amehifadhiwa hospitali ya Amana anakopatiwa matibabu na misaada midogo kama chakula.Cha kusikitisha zaidi baada ya kupimwa kakutwa na Ujauzito wa miezi mitatu na kapimwa virusi vya UKIMWI ambapo Vipimo vinatoka leo alhamisi kujua kama kaathirika au la.

Baada ya leo nitakupa jibu nini kimeendelea kuhusu vipimo na jinsi ya kumpa  msaada binti huyu. Pia unaweza kumsikiliza leo Alhamisi na kesho kupitia Radio Times ndani ya kipindi cha  Hatua Tatu.


Source: mamuafrica

Read More »

JAMANI JAMANI ONA HAYA MAAJABU WATU WANNE WAMBAKA PUNDA HADI KUPOTEZA MAISHA

0 comments


Huko Kamahuha, Maragua nchini Kenya kumetokea tukio ambalo liliwashangaza sana wakazi wa eneo hilo baada ya kukuta maiti ya Punda aliyedaiwa kubakwa mbaka kufa na watu wanne wenye njaa ya ngono.

Tukio hilo lilitokea usiku wa manane karibu na kanisa, amapo watu wa eneo hilo la Kamahuha walikimbia kwenye kituo cha polisi na kutoa taarifa juu ya kitendo hicho kilichofanywa na wanaume wanne walionekana usiku huo wakiwa wamemning'iniza punda huyo juu ya mti na kuanza kumfanyia kitendo hicho cha ajabu.
Pia walikuta kondomu zilizotumika karibu na maiti ya Punda huyo huku akiwa amefungwa miguu yote ya nyuma.
Viongozi wa eneo hilo la Maragua wamelaani sana kwa kitendo hicho ambacho wamekiita ni cha Kishetani, pia wamedai wamekuwa wakiwaita wakazi wa eneo hilo na kuwasihi waachane na matendo hayo machafu ambayo mengi upelekewa na utumiaji wa pombe na madawa ya kulevya.

Read More »

MGONI AKATWA MIGUU YOTE MIWILI BAADA YA KUNASWA AKILA URODA NA MKE WA MTU HUKO KILOSA....MADAKTARI WASEMA HATATEMBEA TENA..!!

0 comments
ALI Omar, mkazi wa Kijiji cha Mabana, wilayani Kilosa, Mkoa wa Morogoro anashikiliwa na polisi kwa kosa la kumkata miguu Said  Iddi kwa kumtuhumu kumfumania na mkewe aliyejulikana kwa jina la mama Ali, mkanda mzima upo mikononi mwa Amani.

Tukio hilo la kikatili lilijiri Julai 15, mwaka huu wakati Said na mama Ali walipokuwa ndani ya nyumba ya Ali iliyopo kijijini hapo.


 Miguu ya Said Iddi ikivuja damu baada ya kukatwa.

MANENO YA SHUHUDA
Akizungumza na mwandishi wetu, shuhuda mmoja ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja alisema Said alifumaniwa ndani ya nyumba asubuhi akiwa na mke wa Ali baada ya kuwekewa mtego ambao ulimnasa vizuri.


 
Mke wa mtu sumu: Said  Iddi akiwa chini baada ya kukatwa miguu na Ali Omar.
Ali alipewa habari na kijana mmoja aitwaye God kwamba mkewe si mwaminifu katika ndoa, akamwongezea kuwa anatoka kimapenzi na Said. Ndipo Ali na mnyetishaji wake huyo walipopanga kumfumania jamaa,” alisema shuhuda.
 
Chini ya ulinzi: Mwenye mali, Ali Omar (kati) akiwa chini ya ulinzi baada ya kumkata Said.
Aliongeza kudai kuwa, Said ni msimamizi wa mashamba ya Ali kijijini hapo na kwamba God ni mtoto wa mwenye nyumba ambayo Ali amepanga kijijini hapo.MPANGO WA FUMANIZI
Habari zinapasha kuwa mara baada ya mnyetishaji kutoa taarifa za usaliti huo, Ali alimtafuta  ‘baunsa’ ambaye jina lake halikuweza kujulikana mara moja na wakaweka mtego kwa kujificha karibu na nyumba hiyo ambayo Said angeingia ili kuivunja amri ya sita ya Mungu.

 
Umbea kazi: Kijana aitwaye God (kulia) aliyetoa taarifa kwa Ali naye akiwa chini ya ulinzi.
Katika kufanikisha mtego huo, mmbeya huyo alipewa jukumu la kuhakikisha nyendo za Said na mama Ali siku hiyo zinarekodiwa mpaka kuingia ndani ya nyumba hiyo na kumtaarifu Ali ambaye siku hiyo alimuaga mkewe kwamba amesafiri.

SAID ATINGA NYUMBANI KWA ALI
Habari zinasema mtoboa siri huyo alimwambia Said kuwa Ali amesafiri na ndipo jamaa akafunga safari kwenda kwa mama Ali kwa nia ya kujivinjari licha ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ukifikia katikati.
Habari zinadai mara baada ya kufika kwa Ali, Said aliingia ndani ya nyumba bila kujua kwamba mwenye mke alikuwa amejificha jirani akisubiri mtego unase.
Inasemekana Said akiwa ndani, Ali na baunsa wake waliibuka kwa kutaarifiwa na God na kumnasa jamaa huyo huku akidai ni mgoni wake. Alimuuliza maswali kadhaa, yakiwemo haya:
Umekuja kufanya nini ndani ya nyumba yangu? Kwa nini umekaa na mke wangu?”
Habari zinasema Said alijibu hakuona ubaya kwa kuwa yeye ni mwangalizi wa mashamba ya mwanaume huyo hivyo anaweza kuingia ndani kwake wakati wowote.

MWENYE MKE ATIBUKA NA MAJIBU, AMWAGA DAMU
Jibu hilo lilidaiwa kumtibua Ali na ndipo yeye na baunsa wake wapomfunga kamba miguuni Said na kuanza kumkata kwa panga mguu mmoja kisha kuugeukia wa pili.
Said alipiga mayowe yaliyowafanya wanakijiji kukimbilia eneo la tukio kwa lengo la kujua kulikoni ambapo walimkuta Said akiwa anavuja damu na sehemu ya nyuma ya miguu ikiwa nyanga’nyang’a.

MWENYE MKE AKIMBIA, ANASWA
Ali, God na baunsa walikimbia eneo hilo. Baadhi ya wanawake walitumia khanga zao kuifunga miguu ya Said kwa lengo la kujaribu kuzuia damu isiendelee kumwagika. Said alikuwa akilia sana.
Wanakijiji walichukizwa sana na ukatili uliofanywa na Ali, hivyo wakaanza kumsaka na kumkamata kichakani akiwa amejificha pamoja na God. Alipewa mkong’oto kwa lengo la kutaka kumuua, lakini viongozi wa kijiji walisihi asiuawe bali afikishwe kwenye kituo cha polisi,” alisema shuhuda.

MKE, MUME, MMBEYA WAFIKISHWA POLISI
Polisi wa Kituo cha Dumila waliitwa na kumchukua Said, Ali na God kwa kutumia gari aina ya Land Rover lenye namba za usajili T 750 AAJ. Mke wa Ali yeye alipelekwa polisi kwa pikipiki.
Walipofika kituoni, Said alipewa fomu ya matibabu ya polisi (PF 3) na kupelekwa Hospitali ya Wilaya ya Kilosa kwa matibabu.
Pale hospitali Said alishonwa miguu yote lakini madaktari wakaamua ahamishiwe katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa matibabu zaidi,” alisema shuhuda huyo.

ANAWEZA ASITEMBEE TENA
Akaongeza: Daktari mmoja alisema haamini kama jamaa (Said) atatembea tena kwa sababu zana iliyotumika kumkata ilifika hadi kwenye mishipa ya nyuma ambayo ndiyo humfanya binadamu aweze kusimama na kutembea.

BAUNSA ASAKWA
Afisa mmoja wa polisi kituoni hapo ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini kwa kuwa si msemaji, alisema wanaendelea kumsaka baunsa aliyeshirikiana na Ali kumkata miguu Said.

SOURCE: GPL

Read More »

TAMAA MBELE: MKE WA NDOA ATAKA KUMUUA MUMEWE NA MTOTO WA MUMEWE ILI ARITHI MALI...!!

0 comments
"Mke wa ndoa inadaiwa ilipanga na majambazi wamuue mumewe ili aweze kumiliki utajiri alionao"
Arusha. Mfanyabiashara wa madini ya Tanzanite mkazi wa Moshono, anadaiwa kutaka kuuawawa na mke wake wa ndoa ili aridhi mali.
Mwanamke huyo alikamatwa na polisi Julai 19 mwaka huu baada ya mpango wake wa kumuua mumewe wa ndoa kwa kutumia majambazi anaodaiwa kuwalipa Sh30 milioni kama malipo ya awali.

Inadaiwa licha ya kutaka kumuua mumewe waliyezaa naye watoto wawili, alipanga kumuua mtoto wa kwanza wa kiume wa mume wake aliyezaa na mwanamke mwingine. Mtoto huyo anaishi mkoani Kagera.

"sikuamini kama itafika siku mke wangu wa ndoa, tena ya Kikristo atafikiria kunitoa roho kwa sababu ya mali, wakati nimempa yeye na familia yake kila wanachohitaji duniani" alisema mwanaume huyo huku akitokwa na machozi.
Alidai kuwa tukio hilo limempa mafundisho tofauti na alivyokuwa anafikiri awali.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas, alipotakiwa kuzungumzia suala hilo hakukiri wala kukanusha kukamatwa kwa wahusika wanne wa mpango huo, lakini alisema atatoa taarifa rasmi baada ya mahojiano na watuhumiwa.

Taarifa za mpango huo zinadai kuwa mwanamke huyo ktk kutimiza azma yake, alimfuata dereva teksi mmoja eneo la Kijenge kumtafutia watu wanaoweza kufanya mauaji hayo.
Inadaiwa dereva huyo aliwasiliana na 'wahusika' na kuwapa mpango huo, lakini mmoja wao hakutaka kushiriki' aliamua kufikisha suala hilo Polisi walioweka mtego na kuwanasa.

Mhusika huyo ambaye hakutaka kutajwa alithibitisha kushirikishwa na kulipwa Sh5 milioni, ikiwa ni malipo ya awali kati ya Sh20 milioni alizoahidiwa.

Hata hivyo, baada ya kukwama mpango wa awali mwanamke huyo aliamua kutimiza azma yake kwa kumtumia dereva teksi huyo huyo kumtafutia wauaji wengine.
Inaelezwa dereva teksi huyo alifanikisha kukodisha wauaji wengine na kuwasafirisha hadi mkoani Kagera kwa ajili ya kufanya mauaji ya mtoto wa kwanza wa kiume wa mume wake aliyezaa na mwanamke mwingine.

Baada ya kupata taarifa hizo, Polisi waliweka mtego na kufanikiwa kuwanasa wahusika wawili mkoani Kagera, hivi sasa wanahojiwa Kituo Kikuu Cha Polisi Arusha.
Polisi baada ya kuwanasa watuhumiwa hao, walianza upelelezi na kufanikiwa kukamata mwingine na mwanamke huyo ambao hadi sasa wanaendelea kuhojiwa.
Inadaiwa baada ya wahusika kunaswa mwanamke huyo alijaribu kutoa Sh50 milioni, ili kuzima sakata hilo, lakini jitihada hizo ziliishia kwenye mtego wa Polisi waliojipanga na kumnasa.
Taarifa za kunaswa kwa mwanamke huyo zilianza kusambaa mwishoni mwa wiki iliyopita, kabla ya kuthibitishwa na mumewe na Polisi.

Read More »

MWANAMKE ALIYEPOTEA KWA MIAKA 50, APATIKANA AKIWA KIKONGWE....!!!

0 comments
 
Royal Canadian Mounted Police (RCMP)

MWANAMKE mmoja aliyepotea kwa zaidi ya miaka 50 mjini Surrey, Columbia amepatikana akiwa hai na kikongwe huku akiwaacha na maswali waliompata kutokana na hali aliyokuwa nayo kwa sasa.
Mwana mama huyo, Lucy Johnson (77) alipotea akiwa na mumewe, Marvin Johnson tangu mwezi Mai, 1965 na taarifa kuripotiwa polisi wa mji huo kwa uchunguzi zaidi. Hata hivyo baada ya juhudi za kumtafuta kushindikana kitengo maalumu cha polisi wa upelelezi kiliamua kumfungulia kesi mumewe juu ya tukio la kupotea kwa mkewe baada ya kuamini anahusika.
Hata hivyo uchunguzi ukiwa unaendelea Marvin alifariki dunia miaka ya 1990 akiwa bado hajahukumiwa juu ya kesi ya upotevu wa mkewe iliyokuwa ikimkabili. Polisi wamekiri kuwa Lucy alipotea tangua miaka 1961 na taarifa zake kuwasilishwa.
Ikiwa ni zaidi ya miaka 50 sasa, Lucy ametambuliwa na mtoto wake wa kike, Linda Evans ambaye wakati mama yake anapotea binti huyu alikuwa na umri wa miaka kati ya saba na nane.
Linda Evans amefanikiwa kumpata mamayake mwezi Juni mwaka huu baada ya safari ndevu ya kumsaka kwa njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutoa matangazo katika magazeti na majarida, hata hivyo amempata akiwa tayari ameolewa na mume mwingine na familia ya watoto wanne.
Evans alishangaa kupokea simu kutoka mjini Yukon kwa binti mmoja ambaye alijitambulisha kuwa mwanamke huyo anayetafutwa pia ni mamayake, hivyo kutaka kujua kama ni yeye au ni mtu mwingine anayefanana majina na yeye.
“…nina maswali mengi ya kutaka kumuuliza mama baada ya kumpata, nafikiri nitakuwa sehemu ya familia…nafikiri nikikutana naye nitamkumbatia na hapo maisha yangu yatakuwa ya mafanikio,” alisema binti huyo akihojiwa na gazeti moja mjini Columbia mara baada ya kupokea simu mamayake amepatikana.
Hata hivyo taarifa zaidi zinasema mama huyo baada ya kuhojiwa anasema hakumbuki kama aliwahi kuolewa na kuwa na familia, kama inavyojulikana.

Read More »

MWENYEKITI WA KIJIJI AMUUA MKEWE KWA KUMNYONGA SHINGO HUKO KAHAMA.....KISA NI WIVU WA MAPENZI..!!

0 comments
MWANAMKE mmoja aitwaye Nyamizi Elias Salamba mwenye umri wa miaka 28 mkazi wa kijiji cha Ilomelo kata ya Ulowa wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, ameuawa kwa kunyongwa shingo na mwanamme anayedaiwa kuwa ni Mwenyekiti wa kijiji cha Kasela wilaya ya Nzega mkoani Tabora.

Taarifa ya jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga imesema tukio hilo limetokea Jumapili ya wiki iliyopita katika kijiji cha Ilomelo wilayani Kahama majira ya saa nne usiku ambapo mwanamke huyo alinyongwa shingo na hawara yake aliyejulikana kwa jina la Kashindye Abeid Sheni mwenye umri wa miaka 45 ambaye ni Mwenyekiti wa kijiji cha Kasela kilichopo mkoani Tabora.

Kamanda wa polisi mkoani Shinyanga, Evarist Mangalla alikitaja chanzo cha mauaji hayo kuwa ni wivu wa mapenzi baada ya marehemu kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamme mwingine ambaye hajafahamika, kitendo ambacho kilimuudhi Mwenyekiti huyo.

Kamanda Mangalla alisema mtuhumiwa anashikiliwa na polisi kwa uchunguzi na atafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.


Read More »

MNYAMA AINA YA KAKAKUONA AONEKANA MAENEO YA BUZA JIJINI DAR..!!

0 comments

Kakakuona akionyeshwa kwa watu walioingia chumbani alipohifadhiwa huko Buza jijini Dar.

Kakakuona akiwa eneo alipohifadhiwa.

Mmiliki wa nyumba alipohifadhiwa Kakakuona, Mweri Swaka akimswalia mnyama huyo.
 
Baadhi wa wananchi wakipozi na Kakakuona huyo.
 
Wananchi wakiingia mmojammoja chumbani kumuona mnyama huyo.
 
Wananchi wakionesha kukasirika baada ya kuzuiwa kuingia ndani kumuona kiumbe huyo.
 
Wananchi wakiwa nje ya nyumba alipo Kakakuona huyo.
KAKAKUONA mwingine ameonekana tena katika maeneo ya Buza jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo ikiwa ni mara ya pili kwa mwaka huu mnyama huyo kuonekana huku tukio la kwanza likianzia Kawe miezi kadhaa iliyopita na hatimaye tukio lingine kujitokeza.


Read More »

MTOTO WA MIAKA 8 AMEJERUHIWA KICHWANI NA KUNG'ATWA KWA MENO MGONGONI NA MABEGANI NA MAMA YAKE MZAZI.

0 comments
Mtuhumiwa huyo akiingia kwenye ofisi ya Mwenyekiti wa mtaa wa Karume kata ya Mnadani
Mtuhumiwa huyo akiwa kwenye ofisi ya Mwenyekiti wa mtaa wa Karume kata ya Mnadani wakati alipokuwa akihojiwa kuhusu tuhuma yake ya kumjeruhi mtoto wake kichwani na mgongoni.
Mwenyekiti wa Mtaa wa Karume kata ya mnadani manispaa ya Dodoma  Matwiga Kyata akionyesha moja ya majeraha ya kichwani na Mgongoni, aliyojeruhiwa mtoto MaggE Fred 8, kipogo hicho kinadaiwa kufanywa na mama yake mzazi.


 



MTOTO Magge Fred 8 amejeruhiwa kichwani na kung'atwa kwa meno Mgongoni na mabegani na Mama yake mzazi kwa sababu aliiba fedha na kununulia Chips bila ruhusa.
Magge alisema anajisikia maumivu makali kichwani na mgongoni baada ya kupigwa na mama yake mzazi kutokana na madai ya yeye kutomwambia Dada yake alipo na chips ambazo mama yake alizikuta chini ya mvungu wa kitanda

tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia jumanne hii, inadawa kuwa Theresia Fidelis ambaye ni mama mzazi wa mtoto huyo alimpiga na kumjeruhi mwanae, mwandishi wetu alishuhudia kovu kichwani la kipigo cha kitu kilichomchana na huku mgongoni kukiwa na majeraha kadha ya meno ambavyo vimemsababishia maumivu makali.

Akiongea mbele ya Mwenyekiti wa mtaa mama wa mtoto huyo alisema aliamua kumpiga kiasi hicho kutokana na mtoto huyo kumfichia siri Dada yake na pia kuiba fedha ndani na kununua chipsi pamoja na matumizi mabaya ya anasa.
Theresia alisema imekuwa ni kawaida kwa mtoto wake huyo Magge Fred 8  kutosema Dada yake alipo na fedha zinazopotea ndani kutojulikana aliyechukua badala yake anaona chipsi na vitu vingine vidogo vidogo vya anasa ndiyo sababu ya kumpiga vibao mpaka kujigonga ukutani na kuchanika kichwani na kumng'ata kutokana na hasira.
.
Mwenyekiti wa Mtaa wa Karume kata ya Mnadani Matwiga Kyata alisema tukio hilo lililpofikishwa ofisini kwake aliamua kuchukua hatua za kisheria na baada ya mahojiano aliamua kuwaita polisi ili sheria ikachukue mkondo wake zaidi.
Baadhi ya akina mama waliokuwepo ofisini hapo kushuhudia tukio hilo walisema mtoto huyo alikimbia toka kwa nyumbani kwao usiku huku akilalama kutaka kuuawa ndipo waka mpeleka kwa mwenyekiti, pamaja na kulaani kitendo alichofanya mwanamke mwenzao.
''We acha hivi unajua uchungu tunaoupata wakati wa kujifungua? kama kweli aliupata angeweza kufanya hivi mpaka kufikia kumng'ata meno akitaka kumnyofoa nyama mtoto wake wala haiingii akili labda akapimwe akili la sivyo achukuliwe hatua kali zinazostahili'', alisema Mwatum Rashid.
Polisi walithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataka wananchi kutoa taarifa mapema pindi wanapoona watoto wakifanyiwa vitendo viovu na wazazi au walezi  wao.

Read More »

BABA AMUUA MWANAE TI KISA AMETAPIKA....!!

0 comments
Mtoto wa miaka miwili amefariki baada ya baba yake kudaiwa kumtupa kitandani - na kusababisha mtoto huyo wa kiume kujibamiza kichwa chake ukutani - kwa sababu alitapika.
Mama wa Jayden Morales Villegas alikubaliana na uamuzi wa kumtoa mtoto huyo kwenye mashine kuokoa maisha Jumapili mchana, siku tano baada ya kudaiwa kupasuka akiwa mikononi mwa baba yake, Angel Villegas, mwenye umri wa miaka 29.

Shambulio hilo linadaiwa kutokea wiki mbili tu baada ya Jayden na kaka zake watatu kutolewa kwenye mikono ya uangalizi wa mama yao na Idara ya Watoto na Familia na kuhamishiwa kwa baba yao.

Villegas, baba wa watoto tisa, alikuwa akimtunza mtoto huyo na baadhi ya ndugu zake kwenye makazi yake huko Homstead, Florida Jumanne ndipo mtoto huyo, ambaye alikuwa akisumbuliwa na baridi, alitapika wakati wa chakula cha usiku.

Alichanganywa na mtoto wake na kumtupa kitandani, kumsababishia mtoto huyo kugonga kichwa chake ukutani. polisi walisema. Alimkuta mtoto huyo akiwa hajitambui siku iliyofuata, kiapo chake kilisema.

Mtoto huyo alikimbizwa katika Hospitali ya Watoto ya Miami, ambako alitangazwa ubongo haufanyi kazi na kuwekwa kwenye mashine ya kuokoa maisha. Lakini alitangazwa kufariki Jumapili Saa 7:30 mchana.

"Inauma mno, alikuwa tu mwanangu," mama wa Jayden, Vanessa Morales alieleza. "Nilimweleza tu awe jasiri, kwamba tunampenda na kaka zake wanampenda na kwamba kamwe sitaweza kumsahau."

Villegas alikamatwa na mashitaka yake yameongezwa kutoka kujaribu kuua hadi kuua na kudhalilisha mtoto kwa kiwango cha juu.

Morales aliongeza kwamba alishitushwa na kukamatwa huko.

"Chizi, anayechukiwa na aliyechanganyikiwa kabisa sababu sikufikiria kabisa angeweza kufanya kitu kama hicho," alisema. "Kwanini hakuelekeza hasira zake kwingineko mbali na mtoto huyo wa miaka miwili, hususani mtoto wake, mtoto wake."

Ukurasa wake wa Facebook ulitawaliwa na picha zake na watoto wake, wakiwamo watoto wawili wa kiume na mtoto wa kike.

Watoto wote wa Villegas na wa Morales wamebaki chini ya uangalizi wa Idara hiyo ya Watoto na Familia.

Villegas anashikiliwa kwa dhamana ya Dola za Marekani 110,000 lakini kama akilipa kiasi hicho, atawekwa chini ya ulinzi nyumbani.

Read More »

HAYA NDIYO YALIYOJIRI MAHAKAMANI KWENYE KESI YA MUME WA JOYCE KIRIA

0 comments
Juzi nikiwa mahakamani Tabora kulia kwangu ni M/Kiti wa Chadema Tabora Kamanda Mbaruk, kushoto ni shemeji yangu Kamanda Bella.

  Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuingia MAHAKAMA KUU ambapo nilishuhudia jaji akifanya kazi yake kwa busara iliyopitiliza (kwa maoni ya Wakili msomi Peter Kibatala) 

Kamanda wangu Mume wangu (kombati nyeusi) na shemeji zangu wakiingia mahakamani jana mjini Tabota. 

Masuala ya Mahakamani yanaitaji subira ya hali ya juu hivyo bado naendelea kumfariji Mpenzi wangu Kilewo ya kwamba mambo haya yatapita tu. zaidi ya hapo namwombea sana.
Kushoto kwangu ni kamanda wa Chadema Tabora (huyu mama) na kulia ni mke mwenzangu (mumewe yupo kesi moja na mume wangu)

Kwa maoni ya Wakili Msomi PK ni kwamba Jaji alichukulia kesi hiyo kwa uzito wake na pia akaheshimu na kuzingatia hali halisi ya Wakili, kwamba anatoka mbali Dar es salaam na hivyo akaamuru Hoja za pande zote mbili zipelekwe kimaandishi kuwaondolea usumbufu hasa wapeleka maombi ambao ni sisi tunaosafiri kila siku. Na kwa sababu hizo basi tar 30july Jaji atataja tar ya uamuzi. 

Asanteni sana sana najua mpo pamoja na familia yetu

Read More »

VIJANA WAUANA JIJINI MBEYA WAKIGOMBANIA PENZI LA MSICHANA

0 comments

Mnamo tarehe 21/07/2012 majira ya saa 23:30hrs huko kijiji cha Nkwangu wilaya ya Chunya mkoa wa Mbeya, Seni s/o Sandu, miaka 20, Msukuma, mkulima na mkazi wa Nkwangu aliuawa kwa kupigwa fimbo kichwani na Tolo s/o Seko, miaka 20, Msukuma, mkulima na mkazi wa Nkwangu.
Chanzo ni ugomvi wa kumgombania msichana aitwaye Holo d/o Kulwa, miaka 16, Msukuma mkulima na mkazi wa Nkwangu.


Mtuhumiwa amekamatwa na taratibu za kumfikisha mahakamani zinaandaliwa.


Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya kamishna msaidizi wa polisi diwani athumani anatoa wito kwa jamii kutojichukulia sheria mkononi kwani ni kinyume cha sheria na kudhibiti hasira zao kwa kuyatatua matatizo ya kimapenzi kwa njia ya mazungumzo ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza.

Signed by, [Diwani Athumani – ACP] kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya.

Read More »

POLISI WAFANIKIWA KUMKAMATA MVUTA BANGI ANALIYEMUUA MDOGO WAKE KWA KUMKATA MAPANGA HUKO SINGIDA

0 comments
 Jeshi la polisi mkoa wa Singida limefanikiwa kumkamata Elibariki Alphoce (21) mkazi wa kijiji cha Kizega wilaya ya Iramba, anayetuhumiwa kumuua mdogo wake Mariam (9) mwanafunzi wa darasa la pili katika shule ya msingi Kizega.

Elibariki anatuhumiwa kumuua mdogo wake Mariam Julai 16 mwaka huu katika kijiji cha Kizega kwa kumkatakata kwa mapanga sehemu mbalimbali za mwili na kisha kuteganisha kichwa na kiwiliwili.

Ilielezwa kuwa Elibariki ni mtumiaji sugu wa madawa ya kulevya aina ya bangi.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Singida ACP Geofrey Kamwela, amesema mtuhumiwa huyo amekamatwa Julai 18 mwaka huu akiwa amejificha kando kando ya mto Ruruma wa kijiji cha Ruruma tarafa ya Kiomboi.

Read More »

DRC: M23 wadai kumshika mateka mwanajeshi Mtanzania.

0 comments
tz c3173


KUNDI la waasi la M23 nchini Drc limedai kumkamata mtu mmoja aliyetambulishwa kwa jina la Christopher George Yohana katika hati yake ya kusafiria akipigana sambasamba na  jeshi la serikali FARDC kupambana na kundi la M23 katika maeneo ya kibati nchini DRC.
Msemaji wa kundi la M23 Vernnei Kazarama ameiambia sauti ya amerika kwa njia ya simu kwamba kijana huyo anayesadikiwa kuandikishwa na serikali ya congo kama mwanajeshi wa Tanzania amejieleza na kukubali kwamba anatokeo nchi jirani ya Tanzania. (HM)

Mapigano yenye ghasia kubwa yalitawala Jumatatu ikiwa ni mwendelezo wa ghasia za mapigano mapya yaliyozuka julai 10 huko kivu kaskazini na kulazimisha maelfu ya watu kukosa makazi na kutorokea nchi jirani ya Uganda.

Kazarama amesema kama serikali ya Tanzania itaomba kuachiliwa mwanajeshi huyo kutoka tanzania kwa njia ya kipiplomasia au kupitia shirika la msaba mwekundi M23 iko radhi kumwachilia huyu mateka huyo.
Hata hivyo ameishutumu nchi ya Tanzania akisema kuwa imekuwa ikiruhusu wapiganaji kutoka Tanzania kusaidiana na vikosi vya serikali ya Congo badala ya wale wa ulinzi wa amani wa umoja wa mataifa.
Jumatatu kundi la M23 ilisambaza hati ya kusafiria yenye majina kamili na utaifa wa mateka huyo ikidai kwamba inataka kutuma ujumbe kwa dunia nzima kwamba Tanzania inaisadia Drc katika uvunjifu wa amani.

Sauti ya ameriba bado inaendelea kuitafuta serikali ya tanzania ili kutoa ufafanuzi zaidi juu ya maelezo yaliyotolewa na kundi la waasi la M23

Read More »

HUYU NDO MSANII WA BONGO MUVI ALIYEJIRUSHA TOKA GHOROFANI NA KUVUNJIKA MIGUU

0 comments

 Msanii chipukizi wa Bongo Muvi nchini Gado Balotel  akiwa mwenye huzuni baada ya kuvunjika kiuno na miguu yote.

  Hapa kama inavyoonekanamiguu ya  Gado Balotel  na bandeji baada ya kuvunjika yote mara baada ya kujirusha toka ghorofa ya 5
  Mshare unamuonesha  Gado Balotel  akiwa kwenye kava la moja ya filamu zake alizocheka kabla ya kukumbwa na balaa hilo.
 Msanii na Kiongozi wa kundi la Bongo Muvi nchini JB ambae ameombwa na wasanii kuchangisha harambee haraka ili kupata fedha za kumsadia msanii mwenzao huyo anaeishi kwa mateso makali.
  Msanii na mwanamasumbwi wa zamani Fike Wilson ambae amepongezwa na wadau baada ya kujitolea kumsaidia msanii huyo, ambapo kwa sasa anaishi nyumbani kwa Fike huku akiwa anabebwa kupelekwa chooni na kurudishwa pia.
  Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania Saimon Mwakifwamba nae pia ameombwa kuungana kwa pamoja na wasanii wengine kumsaidia msanii mwenzao anaishi kwa mateso makubwa usiku na mchana.
Na Livingstone Mkoi

Msanii nyota toka kiwanda cha muvi za kibongo nchini Maulidi Mfaume maarufu kwa jina la Gado Balotel sasa amekumbwa na balaa la aina yake baada ya kuvunjika miguu yote miwili pamoja na nyonga kuteguka baada ya kudondoka toka ghorofa ya nne alipokuwa akiigiza filamu ya msanii mwingine aitwae Baga.

 

Baada Xdeejayz na kituo cha luninga cha DTV kupata taarifa hizo lilipiga hatua ndefu hadi mahala anapojiuguzia msanii huyo ambako ni nyumbani kwa msanii Wilson Fike maeneo ya Home Alone Vijana Kinondoni na kuonana uso kwa uso na msanii huyo aneishi kwenye maumivu makali.

 

Akiongea na mwandishi wetu nyumbani hapo Balotel alisema alikutwa na balaa hiyo wiki mbili zilizopita akiwa Location ndani ya hotel ya Con Way iliyopo Magomen Kagerana wasanii wenzake kama Hemed, Baga, Manaiki Sanga na wengineo wakati wakiigiza.

 

Balotel aliendelea kusema kuwa wakati shughuri za kuigiza ziliendelea na kuna sini moja iliyokuwa inahitajika kuigizwa kwa mfano ikimtaka mtu aigize kama anataka kujirusha kwenye ghorofa lakini asiruke ili kameraman  kuchukua picha achukue shoti hiyo kisha mtu huyo aende chini kisha achukuliwe shoti nyingine ya kujifanya ametua chini.

Msanii huyo aliendelea kusema kuwa nafasi hiyo ilibidi aigize msanii mwenye filamu Baga lakini kutokana na uwoga wa msanii huyo alikuwa akijishauri namna ya kuigiza kuruka ghorofani ndipo Ballotel akamtoa pembeni na kumuonesha namna ya kuruka kama Jet Lee huku akimwambie mwenzake hiyo ilikuwa kazi ndogo sana.

 

Msanii huyo aliendelea kusema kuwa baada ya hapo alijikuta ameruka toka ghorofa ya nne, lakini aliendelea kusema“ Wakati nikiwa bado sijashuka chini njiani nilianza kuhisi harufu ya kifo kwani tayari nimuona Israel mtoa roho akinipungia mkono na hatimae nilitua chini  kwa kufikia miguu” Alisema  Ballotel

 

Hata hivyo kijana huyo aliongeza kusema kuwa mala baada ya kutua nchini alihisi moto unawake miguuni mwake huku harufu ya damu ikimtoka puani na mdomoni na baada ya kujiangalia aliona visigino vyake vikiwa vimepasuka vyote huku tumboni kukiwa na maumivu makali sana kumbe wakati huo nyonga ilikuwa imeachia huku miguu yake ikiwa imesogea tumboni.

 

Gado alisema baada ya tukio hilo wasanii wenzake walimchukua na kukmimbiza Hospital ya Mwananyamala mbapo dakika chache baadae walimkimbiza Muhimbili kwa matibabu zaidi.Msanii huyo ambae ametamba sana kwenye filamu kama Going Bongo,Msitu wa Hifadhi,Tumbo Joto na Escap ambayo alikuwa akiigiza siku ya tukio lililomkuta.

Aidha msanii huyo aliendelea kusema kwa sasa anaishi kwenye mateso makali huku wasanii wenzake wakishindwa kumpa ushirikiana “Hapa nilipo nalelewa na Fike Wilsoni ndiye anaenibeba kwenda chooni na kunirudisha kwa kweli hali yangu sio nzuri nahitaji msaada wa wasanii wenzengu, Wako wanaokuja kunirushia chochote kama

 

Kalapina,Young Killer na madaktari wanasema huenda wakanishauri kwenda India ili wakazirekebishe nyonga zangu” Alisema Gado na kuongeza kuwa anawaomba wasanii wenzake wasamalia wema kumsaidia kwani hali yake ni mbaya na huenda kwa mujibu wa madakatari wake akahitajika kupelekwa India ili kukinusuru kiuno chake la sivyo hatozaa tena kwa vile nyonga vimeshafyatuka.


Read More »

MASKINI WATOTO HAWA WANAUZWA,KILA MMOJA 1,000,000.

0 comments
 
Na  Juma Kapipi, Tabora
MAHAKAMA ya Mkoa wa Tabora imemhukumu kifungo cha mwaka mmoja jela na faini ya shilingi laki moja (100,000/=) raia wa Burundi, Emmanuel John (22) kwa kosa la kuingia nchini kinyume cha sheria.
Hivi karibuni, Maafisa wa Idara ya Uhamiaji mkoani hapo walimkamata Emmanuel kwa kosa la kuingia nchini kinyume cha sheria akiwa na watoto sita aliotaka kuwauza shilingi 1,000,000 kila mmoja.

 
Mbele ya Hakimu Mkazi Jackton Rushwela,  kijana huyo alikiri kosa la kuingia nchini kinyume cha sheria lakini alikana kosa la kuingiza watoto kwa nia ya kuwauza.
Kutokana na kukiri kosa la kwanza, Hakimu Rushwela
alimhukumu kifungo cha mwaka mmoja jela na faini ya shilingi laki moja.
Kuhusu shitaka la kusafirisha binadamu, upande wa mashitaka ulidai mshitakiwa alikamatwa akiwasafirisha watoto Ndayisenga Batiliza (13),
Ndakusenga Emmanuel (15), Nimbonajile Nagenda (13),
Yazid John (15), James Justus (14) na Samson Banteke(17).
Baadhi ya watoto hao walitoa ushahidi mahakamani kwamba walisafirishwa na mshitakiwa Emmanuel John kutoka Burundi na Rwanda hadi walipokamatwa eneo  la  Ulyankulu  wilayani Kaliua mkoani hapa.
Kesi ya kutaka kuwauza watoto imeahirishwa hadi Julai 25, mwaka huu itakaposikilizwa tena kwa mashahidi wengine kutoa ushahidi wao.

Read More »

WALIOWAUA WANAJESHI WA TANZANIA WATAJWA.....NI KUNDI LA "JANJAWEED" LINALOUNGWA MKONO NA SERIKALI YA SUDAN

0 comments
WAKATI miili ya wanajeshi saba ikiwa imeagwa jana katika Viwanja vya Makao Makuu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania, imeelezwa kuwa kundi la Janjaweed linaloungwa mkono na serikali ya Sudan ndilo lililowavamia na kuwaua askari hao nchini humo  na kuwajeruhi wengine 17 .
Wanajeshi hao wa Tanzania ambao walikuwa ni sehemu ya Jeshi la Kulinda Amani la Umoja wa Mataifa (Unamid), walifanyiwa unyama huo Julai 13, mwaka huu katika eneo la kusini mwa Darfur, nchini Sudan.

Kiongozi wa moja ya makundi ya wapiganaji la Sudan Liberation Movement (SLM), Minni Mannawi ameibuka na kuwatuhumu wanamgambo wa Janjaweed wanaoungwa mkono na serikali ya nchi hiyo na ametaka ufanyike uchunguzi wa kimataifa.
Katika mahojiano yake na Gazeti la Sudan Tribune alipokuwa anahudhuria mkutano wa majadiliano kuhusu namna ya kupata amani ya kudumu nchini Sudan uliofanyika jijini Geneva Uswisi wiki iliyopita, alikanusha kuwa kundi lake linahusika na shambulio hilo.
 



“Tuna uhakika shambulio lililofanywa dhidi ya walinzi wa amani wa Unamid liliandaliwa na kutekelezwa na Janjaweed, tuko tayari kutoa ushirikiano kwa chombo maalum cha kimataifa kitakachoundwa kufanya uchunguzi kuhusu tukio hili…Nashauri serikali (ya Sudan) isishiriki katika uchunguzi kwa sababu itaficha ukweli,” alisema Mannawi.

Aliongeza kuwa wanamgambo hao waliowashambulia wanajeshi wa kulinda amani hivi sasa wanakabiliwa na ukata wa hali ya juu na kukosa vifaa kwa sababu serikali haina tena uwezo wa kuwahifadhi, hivyo wameamua kufanya matukio ya uporaji kukidhi mahitaji yao.
 
Msemaji wa Katibu Mkuu wa UN, Martin Nesirky alisema wameanza kufanya uchunguzi wao binafsi. Taarifa ya UN ilieleza juzi kuwa mashuhuda wamekuwa wakieleza mauaji hayo yamefanywa na kundi linaloungwa mkono na serikali ya Sudan.
Wakati huo huo, majeshi ya Nigeria yamejitoa kulinda amani Darfur. Hazikutolewa sababu za kufanya hivyo japokuwa UN imethibitisha.


Read More »