Mzee Small anateseka-1
![]()  | |
| Anachechemea huku mkono wa kushoto akiwa ameufumbata kwapani, uso umekumbwa na maumivu yanayoshindana na tabasamu hafifu analojaribu kulitoa. | 
ANAFAHAMIKA zaidi kwa jina la Mzee Small, lakini jina lake halisi ni Small Wangamba.
                               Ana sifa nyingi, lakini iliyo kubwa ni ucheshi,  uchangamfu, ukarimu na kila aina ya bashasha. Hata hivyo kwa sasa hali  yake ni tofauti, mambo mengi yamebadilika.
                               Sipati shida kumpata pale nilipokusudia kumfikia  na hata ninapofika nyumbani kwake katika banda la vyumba viwili ambavyo  vimemalizwa kujengwa hivi karibuni, napokewa na msichana  anayenikaribisha katika kiti nje ya kibanda hicho.
                               Ujumbe unapelekwa ndani kwa Mzee Small kuwa ana  mgeni na dakika 20 baadaye mlango unafunguliwa, anachomoza mtu ambaye  sipati taabu kumfahamu kuwa ni Mzee Small, mwigizaji nguli ambaye  maradhi yamemkalisha kitako.
                               Anachechemea huku mkono wa kushoto akiwa  ameufumbata kwapani, uso umekumbwa na maumivu yanayoshindana na tabasamu  hafifu analojaribu kulitoa.
                               Hali hiyo inaakisi wimbo mmoja wa Shakila Abdallah  ‘Bi. Shakila’ wenye mashairi ‘Macho yanacheka moyo unalia’. Kimsingi  Mzee Small anaumwa ingawa anajaribu kutabasamu, kinachoonekana katika  paji lake la uso ni tofauti na tabasamu hafifu analojaribu kulitoa pale  macho yetu yanapogongana na wakati wa mazungumzo anabainisha  kinachomsibu.
                               “Sipo vizuri, naumwa. Kwa sasa inawezekana  ikaonekana kama nina nafuu kidogo, lakini naumwa,” anasema baada ya  kunikaribisha katika chumba kimoja ambacho anakimiliki na mkewe.
                               Chanzo cha tatizo
                               Anasema tatizo lake lilimuanza Mei mwaka jana  baada ya kurudi kutoka Mwanza alikokuwa na kazi ya kutumbuiza katika  tamasha la kupambana na mauaji ya Albino. Tamasha hilo liliratibiwa na  Kituo cha Under The Same Sun .
                               “Nilitoka Uwanja wa Ndege (Dar es Salaam) na  kufika hapa nyumbani, nikaingia chooni moja kwa moja. Lakini wakati  natoka, nikadondoka. Nilipojitahidi kunyanyuka haikuwezekana hivyo  nikabebwa hadi chumbani,” anasema.
                               Anasema akiwa chumbani alijaribu kujinyanyua  akajikuta anadondoka tena, hivyo akawahishwa hospitali moja jirani na  nafuu haikupatikana.
                               Ikalazimika apelekwe Hospitali ya Amana jijini Dar  es Salaam ambako alilazwa siku tatu kabla ya kuhamishiwa Hospitali ya  Taifa ya Muhimbili.


0 comments: